.
Msanii wa Hip pop Ney wa mitego 'TRUE
BOY' Amewaonyesha uso wa mbuzi Basata ambao awali walimwonya kutokana na
tabia yake ya kuvaa mlegezo "KATA K" akiwa jukwaani kwa madai ya kuidhalilisha sanaa hiyo.
Katika hali ya kushangaza kabisa Msanii
huyo ameonekana kupuuzia agizo hilo la basata na kendelea kuvaa mlegezo
wakati akilishambulia Jukwaa huku akishangiliwa na mashabiki lukuki wa
Bongo Fleva .
Tukio hilo lilitokea jana wakati wa Show ya FIESTA DAY 2 iliyofanyika kwenye viwanja vya Leaderz Club alipokuwa akiwapagawisha wapenzi wake na kibao chake cha "MUZIKI GANI" Akiwa sambamba na Msanii mwenzake Diamond Platinumz.
Tukio hilo lilitokea jana wakati wa Show ya FIESTA DAY 2 iliyofanyika kwenye viwanja vya Leaderz Club alipokuwa akiwapagawisha wapenzi wake na kibao chake cha "MUZIKI GANI" Akiwa sambamba na Msanii mwenzake Diamond Platinumz.
Sasa wapenzi wa Bongo fleva wanasubiri Rungu la Basata liweze kufanya kazi yake huku wengi wakionekana kumtetea kwa kudai kuwa kila mtu ana aina ya maisha yake 'Life Style'
0 comments:
Post a Comment