Mwimbaji
wa ‘Fine China’ Chris Brown, ametupwa selo za polisi huko Washington,
D.C, baada ya kumpiga mtu mmoja asiyemfahamu na kumjeruhi usoni.
Kwa mujibu wa TMZ Chris na mlinzi
wake walikamatwa jumapili asubuhi, na kwamba Chris alimpiga ngumi usoni
mtu huyo majira ya saa kumi na nusu alfajiri nje ya hotel baada ya
kutokea hali ya kutoelewana kati yao.
Mtu huyo aliyepigwa na Chris
aliiambia TMZ kuwa ngumi ya Chris imepasua pua yake na inambidi leo
(jumatatu) aende hospitali kufanyiwa upasuaji.
Amesema yeye sio shabiki wa Chris na
alikuwa anawapiga picha wasichana wawili ambao walikuwa wanapiga picha
mwimbaji huyo nje ya hotel, na haelewi ni kwa nini Chris alikuwa kichaa
vile na kumshambulia.
Hata hivyo mtu huyo amesema angeweza
kumsamehe Breezy kama angeomba msamaha pale pale, lakini sasa hivi
atamfunguliaa kesi dhidi yake na tayari ameshampata mwanasheria.
Lakini chanzo ambacho kiko karibu na
Chris Brown kimesema kuwa mtu huyo hakuwa anataka kupiga picha nje ya
hotel, bali alikuwa anataka kuingia kwenye ‘tour bus’ ya Chris ili apige
picha akiwa ndani, na mwimbaji huyo alikuwa anajaribu kumzuia.
Kwa mujibu wa sheria za Washington, D.C, endapo Chris atapatikana na hatia anaweza kufungwa jela miaka minne.
Tukio hili linamuweka matatani zaidi
mwimbaji huyo ambae bado yuko katika probation ya adhabu aliyopewa baada
ya kumpiga mpenzi wa zamani ‘Rihanna’mwaka 2009.
Hii inaweza kutumiwa na mahakama kuwa Breezy amekiuka masharti ya probation hiyo.






0 comments:
Post a Comment